Tuzo la Mabingwa wa Dunia hutuza watu binafsi, makundi na mashirika ambayo juhudi zao huathiri mazingira kwa njia chanya. Washindi wa mwaka wa 2023 wanatekeleza masuluhisho na sera za kukomesha uchafuzi wa plastiki .
Kila mwaka tangu mwaka wa 2005, UNEP hutuza watu binafsi na mashirika yanayofanya kazi kupata masuluhisho bunifu na endelevu ya kushughulikia changamoto za aina tatu duniani za mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa mazingira na bayoanuai, na kemikali, uchafuzi na taka. Mabingwa hubadilisha uchumi wetu, huvumbua, huongoza mabadiliko ya kisiasa, hupambana na ukosefu wa haki ya mazingira na kupigania malighafi zetu.